1 Samuel 3:1-6

Bwana Amwita Samweli

1 aKijana Samweli alihudumu mbele za Bwana chini ya Eli. Katika siku zile neno la Mungu lilikuwa adimu, hapakuwepo na maono mengi.

2 bUsiku mmoja Eli, ambaye macho yake yalikuwa yamefifia sana kiasi kwamba aliona kwa shida sana, alikuwa amelala mahali pake pa kawaida. 3 cTaa ya Mungu bado ilikuwa haijazimika, na Samweli alikuwa amelala Hekaluni
Hekaluni maana yake ndani ya Maskani ya Bwana.
mwa Bwana, ambapo Sanduku la Mungu lilikuwako.
4 eKisha Bwana akamwita Samweli.

Samweli akajibu, “Mimi hapa.”
5Naye akakimbia kwa Eli na kumwambia, “Mimi hapa, kwa kuwa umeniita.”

Lakini Eli akasema, “Sikukuita; rudi ukalale.” Hivyo akaenda kulala.

6Bwana akaita tena, “Samweli!” Naye Samweli akaamka, kwenda kwa Eli na kusema, “Mimi hapa, kwa kuwa umeniita.”

Eli akasema, “Mwanangu, sikukuita, rudi ukalale.”

Copyright information for SwhKC